Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, maelfu ya wananchi wa Australia siku ya Jumatatu walifanya maandamano katika uwanja wa eneo la kibiashara la Sydney; maandamano hayo pia yaliendelea kwa kiwango cha kikanda katika miji na wilaya mbalimbali kote Australia.
Tume ya Australia katika Baraza la Amnesty International ilisema: “Herzog kwa zaidi ya miaka miwili ameleta mateso na misiba mikubwa juu ya Wapalestina na watu madhulumu wa Ghaza; anafanya vitendo hivi kwa ujasiri na kwa kinga kamili. Hatuwezi kubaki kimya.”
Baraza la Wayahudi wa Australia pia ni miongoni mwa wakosoaji wakuu wa serikali ya Israel, na siku ya Jumatatu lilichapisha barua ya wazi iliyotiwa saini na zaidi ya Wayahudi 1000 wasomi wa Australia na viongozi wa jamii, likimtaka pia Albanese afute mwaliko wa Herzog.
Vita na mauaji ya kimbari ya Israel huko Ghaza vimesababisha zaidi ya Wapalestina 72,000 kuuawa na utawala huo wa umwagaji damu; bado makumi ya maelfu ya miili isiyo na uhai imekwama chini ya vifusi vilivyosababishwa na vita na haijahesabiwa.
Chanzo: Al Jazeera
Maoni yako